UHAKIKI WA RIWAYA YA TAKADINI

UHAKIKI WA RIWAYA

TAKADINI 2004

MWANDISHI – BEN J. HAMSONI

MCHAPISHAJI – MATHEWS BOOK STORE AND STATIONERS

Riwaya hii ya TAKADINI inahusu mila na desturi za kiafrika hasa za kuua MAALBINO (watu wenye ulemavu wa ngozi).

*Mwandishi ameonesha jinsi mila hizi zilivyopitwa na wakati na kutaka jamii za kiafrika ziachane na mila hizi kwani hurudisha nyuma maendeleo:

Mwandishi anaonesha jinsi Sekai alivyo a mzaa TAKADINI (SOPE) na kusababisha atoroke katika kijiji kile ili kumnusuru Takadini asiuwawe.

1.MAUDHUI

DHAMIRA KUU – UKOMBOZI WA KIUTAMADUNI

Mwandishi anaonesha jinsi jamii zinavyokumbatia mira na desturizilivyopitwa na wakati hasa zile zinazomkandamiza mwanamke na mtoto katika ndoa, mirathi, utu, elimu uhai maamuzi, magawanyo ya kazi na mapato.

Mwandishi anaeleza jinsi jinsi mila hizi potofu zinavyohatarisha maisha ya watoto walemavu kama Takadini, kijana aliyezaliwa akiwa zeruzeru ambaye jamii yake iliazimia kumuua siku ya pili baada ya kuzaliwa mwandishi anasema.

           “Sekai alimpenda Makwati siku zote, na sasa anamuacha aamuliwe na wazee kwa sababu

ameshindwa kumpatia aina ya mtoto yetaka ……. Katika kijiji hiki zeruzeru hakuwa na nafasi

              (uk 12) “

Hapa tunaona jinsi wazee wa kijiji hiki walivyokuwa wasimamizi wakuu  wa mila na desturi mbaya hali iliyosababisha Sekai atoroke ili kuponya maisha ya Takadini yasiangamizwe nay eye pia kama Makwati anaposema.

                  “Lakini Sekai endapo wataamua mtoto auwawe hata nay eye atauawa kwa sababu ya

kupinga sheria za kale “

Hivyo basi hatuna budi kuachana na mila zilizopitwa na wakati na kuanza kutetea haki, uhuru na utu wa watu dhidi ya mila na desturi.

Mwandishi anamuonyesha Sekai jinsi anavyokuwa jasiri kwa kupinga mila potofu zilizopitwa na wakati kwa kutoroka na Takadini ili kukwepa adhabu ya kifo ambayo wangeipata.

                    “Sekai alikwisha amua lazima aondoke asubuhi itakayofuata kulilia uhai wa watoto wake”

Pia msanii anaonesha jinsi mila na desturi zinavyojitokeza kwenye ndoa pale Shingai anapochaguliwa mtu kumuoa.Wazazi walimkatalia asiolewe na Takadini ila aolewe na Nhano mvulana jasiri lakini msichana huyuhuyu anataka kuchaguliwa mtu wa kumuoa na wazazi wake na kuolewa na Takadini.

Msanii anamchora Shengai akiwaeleza wazazi wake :-

                   “Huyu ndiye mtu anayetaka anioe, wewe na baba mlikuwa na hamu ya kuniozesha kwa nyumba ya Manyamombe hafuati matakwa yangu hayakusikilizwa (uk 118)

Hivyo mwandishi anaonyeshaa kuwa ni sisi wenyewe tunaotaka kupambana na mira na desturi zilizopitwa na wakati kama Shingai na Takadini walivyoleta mabadiliko katika jamii . Tendai anashuhudia hilo na kusema.

“Wewe na Takadini mmebadilisha mambo mengi kijijini hapa kwa sasa sifikirii kwamba kuna mtu yoyote atakayekuwa na moyo wa kuwaharibu watoto wachanga masopeau wenye ulemavu. Ahsante nyinyi kwako na Takadini kwa baba Chivero (uk 126)

Hivyo msanii anaonesha jinsi watu wanavyotakiwa kupinga mila potofu ili kuleta ukombozi katika jamii.

DHAMIRA NDOGONDOGO

1. NDOA. Ni makubaliano kati ya watu wawili wanaokubaliana ila tunaona mila na desturi zinaingilia

maswlawa ya ndoa.

             Shingai analazimishwa kuolewa na Nhamo wakati Shingai alikuwa hampendi pale anaposema

             “Nataka waniache peke yangu ili niamue mwenyewe (uk115)

 

2. MAPENZI.Katika riwaya hii kuna mapezi ya kweli nay a uongo.

                    Mapenzi ya dhati kati ya Takadini na mamae, Takadini na mzee Chivero, Takadini na

                    Shengai, Sekai na Pindai na Sekai na Mzee Chivero. Shengai anasema kuwa” huyu ndiye

mtu ninayetaka anioe…. Wewe na baba mlitaka kuniozesha katika familia ya Manyambe”

                    (uk118)

                     Sekai alimpenda Takadini hasa pale anapomwambia makwati kwa………………

 

                            “Ni mtoto wangu wa kwanza niliyemsubiri kwa miaka mingi siwezi kukubali

kumpoteza la humtaki nirejeshe kwetu nitajitoa mhanga kwa ajili yake” (uk 11)

Chiveri alimkaribisha Sekai katika kijiji chake . Chivero na Takadini walipendana sana kwani alimfundisha namna ya kufahamu mitishamba na uwindaji.

Ø  Mapenzi ya uongo ni kati yam zee Makwati kwa Sekai baada ya kujifungua mtoto zeruzeru.

Ø  Mapenzi kati ya Dadirai na Bumbidzui kwa Sekai jinsi walivyokuwa wakimsengenya.

3.DHANA POTOFU

Jamii nyingi za kiafrika zinaamini mila potofu zilizopitwa na wakati ikiwa ni pamoja na kuwaua zeruzeru mfano Mapunzure anasema “matoto lazima auwawe” (uk 35)

 

4.  UMOJA NA USHIRIKIANO

Mwandishi anasisitiza kuwa ili kupiga vita mila potofu ni lazima kuwa na umoja na ushirikiano. Mzee Chivero, Tendai na Mtemi Masasi walishirikiana kumlina Takadini dhidi ya unyanyapaa. Mzee Makwatianasema “sasa kinajua sope hawezi kuzaa sope”

5.UJASIRI

Msanii anasema ujasiri ni silaha mojawapo katika kuleta uokombozi dhidi ya  mila potofu. Mfano Sekai alikuwa jasiri kutoroka ili Takadini asiuawe, Shengai alikuwa jasiri kukataa kuolewa na Nhamo (Mchumba aliyechaguliwa na mzazi wake)

 XXXXXMCHAMBUZI MWL MKAMBA. BAED (HONS) UDMS 2009XXXXX

 Inaendelea=======>


Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER MKAMBA EDUCATION CONSULTANCY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment:

Post a Comment