TAMTHILIYA: NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE

UHAKIKI WA TAMTHILIYA 

TAMTHILIYA: NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE

MWANDISHI: EDWIN SEMZABA

MWAKA: 1988

MCHAPAJI: DAR ES SALAAM UNIVERSITY PRESS

UTANGULIZI                                              

 

   Ngoswe penzi kitovu cha uzembe ni tamthiliya inayochambua haki halisi ya kijijini namna watendaji wanavyoshindwa kuwajibika katika kuleta maendeleo ya kijamii sehemu za vijijini .

Mwandishi anaonesha namna Ngoswe anavyoharibu kazi ya sense kwa uzembe wake wa kuchanganya mapenzi na kazi pia anaonesha hali duni za maisha katika sehemu za vijijini, kukosekana kwa huduma kama vile shule, hospitali ni kikwazo kikubwa sana katika maendeleo.

 

MAUDHUI

DHAMIRA KUU:KUCHANGANYA MAPENZI NA KAZI

Mwandishi wa tamthiliya hii ameliweka suala hili kuwa kitovu cha uzembe. Mwandishi ametuonesha Ngoswe akiwa na uchu wa mapenzi mara amwonapo mazoea. Tatizo la Ngoswe halikuwa kupenda bali kushindwa kudhibiti penzi lenyewe na kusababisha kuharibika kwa kazi ya sense kwa kuikosesha serikali kumbukumbu za baada. Hivyo msanii anaiasa jamii kutochanganya mapenzi na kazi kwani huwezi kuwatumikia mabwana wawili.

DHAMIRA NDOGO NDOGO

i)        ATHARI ZA ULEVI: Mwandishi ametuonesha kuwa suala la ulevi ni chanzo cha uzembe kazini. Mtunzi wa tamthiliya hii amewatumia Ngoswe na mito mingi wanaojihusisha na ulevi wa pombe za mnazi wakati wa kufanya kazi ya sense. Ulevi huo ulisababisha uzembe na hatimaye mito mingi anaamua kuchoma kazi ya sense.hivyo msanii anataka jamii kuacha ulevi kwani huathiri uwajibikaji kazi.

ii)      UMUHIMU WA ELIMU : mwandishi wa tamthiliya hii ametuonesha kuwa watoto wengi hawasomi kwa sababu shule ziko mbali. Hivyo jamii haina budi kujenga shule karibu ili kila mtoto apate elimu.

Vilevile mtunzi ametuonesha mitomingi akiwa na dhana potofu juu ya elimu kwani anasema wazee wengi hawasomagi wasome nyie vijana. Elimu haina mzee wala kijana kwani elimu haina mwisho, hivyo kila mtu anafrsa ya kusoma.

 

     Pia msanii anatuonesha kuwa endapo elimu itatumika vibaya, basi inaweza kuleta madhara makubwa kwa jamii. Mwandishi ametuonesha Ngoswe aliyekuwa na Elimu ya kutosha anashindwa kuleta ufanisi wa kazi ya sense. Hivyo ili elimu iweze kuwa ya manufaa ni lazima itumike katika kuibadilisha na kuisukuma mbele jamii katika suala zima la maendeleo.

iii)    IMANI ZA KISHIRIKINA: mwandishi ametuonesha Mama jane akikataa kuhesabiwa kwa sababu ya imani za kishirikina kwani anadai kuwa ukituhesabu watoto wa watu ili awaroge. Hivyo msanii anaitahadhalisha jamii kuwa imani za kishirikina hazina nafasi katika kuiletea jamii maendeleo

iv)    MALEZI NA NDOA ZA MITARA: mwandishi wa tamthiliya hii ametuonesha mama mazoea anajihusisha na malezi ya mazoea ingawa kulikuwepo na mwingiliano kutokana na mitomingi kuendekeza ndoa za mitara. Hivyo kusababisha wake zake kutokuelewana katika suala la ,alezi ya  mazoea.; hivyo mtunzi anaiasa jamii kuepuka ndoa za mitara kwani huweza kusababisha kutokuwepo kwa utulivu katika familia.

v)      ATHARI ZA UVIVU : mwandishi wa tamthiliya hii ametuonesha kuwa kijiji cha Ngengemkeni kinaelekea kuwa na watu wengi walevi suala hili linaathiri kazi zote zinazohusu watu na kusababisha jamii kutokupata maendeleo. Watu wanajihusisha na ulevi kuliko kufanya kazi, hali inayopelekea kuwepo kwa umasikini katika jamii. Hivyo jamii lazima iachane na uvivu kwani ni sumu ya maendeleo.

vi)    NAFASI YA MWANAMKE KATIKA JAMII : mwandishi wa tamthiliya hii amemchora mwanamke katika nafasi zifuatazo.

Ø  Mzazi na mlezi, mwandishi ametuonesha mama mazoea akijihusisha na malezi ya mwanae ingawa mazoea alitoroshwa na Ngoswe. Hivyo ni jukumu la wazazi wote kuwapa watoto wao malezi.

Ø  Kiumbe duni, mwandishi ametuonesha mitomingi akiwafananisha wakeze na mazoea kwa kusema kuwa akili zenu ni sawa na za mazoea. Hii inaonesha kudharauliwa kwa mwanamke tabia ambayo Haifa katika jamii

Ø  Chombo cha starehe, mwandishi amemchora mwanamke kama chombo cha starehe baada ya kuwaonesha mitara,mfano mitomingi aliyekuwa na wake wawili. Mama mazoea na mama mainda. Hivyo wanaume hawapaswi kuwatumia kwa ajili ya kukizi haja zao bali wawathamini.

Ø  Mwepesi wa kushawishika; mwandishi ametuonesha mazoea anakubali kutoroshwa na Ngoswe ilihali alikuwa na mchumba tayari. Hivyo mwandishi anaiasa jamii hususani wanawake kuwa waaminifu.

 

vii)  MIVUTANO YA MAADILI YA MJINI NA KIJIJINI: mwandishi wa tamthiliya hii ametuonesha tofauti za kiutamaduni kati ya maisha ya mjini na kijijini. Mtunzi ametuonesha mivutano ya kimaadili, kitendo cha Ngoswe kumtorosha mazoea bila ridhaa ya wazazi ni kinyume na taratibu za vijijini lakini ni jambo la kawaida kwa upande wa mjini. Hivyo msanii anasisitiza maisha ya kijamaa yadumishwe mjini ili maadili mema yatawale .

 

 

  Huu ni mwelekeo wa imani ya mwandishi kuhusu maisha. Msanii anaamini kuwa jamii inaweza kuingia katika matatizo pindi inapochanganya vitu viwili kwa wakati mmoja. Vilevile msanii anaamini kuwa ubora wa maisha ya watu kutokana na watu kuishi kijamaa. Hivyo ujamaa ndio utakaomaliza matatizo mbali mbali katika jamii.

 

 

MSIMAMO / MITAZAMO

   Hii ni hali ya mwandishi kuamua kufata na kushikilia jambo Fulani. Mwandishi wa tamthiliya hii ana msimamo wa kimapinduzi kwani wamezungumzia wazi juu ya matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii na kuonesha uhalisia wake.matatizo haya ni umaskini, ulevi, elimu, ndoa za mitara. Hivyo mwandishi anaonesha suluhisho la matatizo hayo ni kuishi kijamaa.

 

UJUMBE

 Ni funzo ambalo msomaji wa kazi ya fasihi hupata baada ya kusoma kazi mbalimbali za fasihi

-       Baadhi ya ujumbe katika tamthiliya ya Ngoswe penzi kitovu cha uzembe ni

i)        Jukumu la malezi katika familia si la mtu mmoja bali ni wajibu wa baba na mama. Hivyo wazazi wote wawili wana jukumu la kumlea mtoto ipasavyo. Ujumbe huu unaibua dhamira ya   malezi katika familia

ii)      Ulevi ni kikwazo cha maendeleo katika jamii. Hivyo haipaswi kuchanganya ulevi na kazi. Mwandishi anaibua dhamira ya Athari za ulevi

iii)    Ni vema shule zijengwe karibu ili watoto waweze kupata elimu kwa urahisi dhamira inayotokana na ujumbe huu ni suala la Elimu katika jamii

iv)    Jamii inapaswa kuachana na dhana ya kumchukulia mwanamke kama chombo cha starehe na mtuduni. Ujumbe huu unaibua dhamira ya  Nafasi ya mwanamke katikajamii

v)      Suala la imani za uchawi na ushirikina linatakiwa kutupiliwa mbali kwani hukwamisha maendeleo katika jamii ujumbe huu unatupatia dhamira ya Imani zakishirikina

vi)    Kupenda si dhambi bali tunapaswa kuzingatia wakati wa kupenda, mahala na nani anayependwa? Msanii anatuasa kuwa mshika mawili moja humponyoka kama ilivyotokea kwa Ngoswe. Ujumbe huu unatupatia dhamira ya Mapenzi

vii)  Mapenzi yasiofuata utaratibu unaokubalika katika jamii ni chanzo cha kuharibu utendaji wa kazi. Hii imejidhihirisha kupitia Ngoswe na mazoea hivyo kuibua dhamira ya mapenzi na kazi.

viii)                     Suala la uzembe linaweza kusababisha umaskini na kutokuendelea katika jamii. Ujumbe huu unaibua dhamira ya Athari za uzembe

ix)    Ni bora huduma za kijamii zitolewe sehemu zote mjini na vijijini, huduma hizi ni kama vile shule, hospitali, maji na umeme. Ujumbe huu unaibua dhamira ya umuhimu wa huduma za kijamii.

 

 

MIGOGORO:

Migogoro ni misiguano/ mivutano au hali ya kuelewana baina ya pande mbili au zaidi katika kazi ya fasihi

   Miongoni mwa migogoro iliyojadiliwa katika tamthilia hii ni pamoja na

·         Migogoro kati ya Ngoswe na wazazi wa mazoea, chanzo cha mgogoro huu kilikuwa kutoroshwa kwa mazoea na Ngoswe bila ridhaa ya wazazi wake hivyo suluhisho la mgogoro huu ulikuwa mbaya kwani mitomingi aliamua kuchoma kazi ya sense.

·         Migogoro kati ya mazoea na wazazi wake, mgogoro huu ulitokea baada ya mazoea kuamua kutoroshwa na Ngoswe wakati tayari alikuwa na mchumba hii ilikuwa kuchomwa kwa kazi ya sense na kusababisha mitomingi kudharau wakeze kwa kusema kuwa wamechangia katika kutoroshwa  kwa mazoea.

·         Mgogoro kati ya Ngoswe na serikali, mgogoro huu ulitokea baada ya Ngoswe kuharibu kazi aliyotumwa na serikali kwa uzembe na mapenzi suluhisho la mgogoro huu lilikuwa kufikishwa kwa Ngoswe katika mikono ya sharia lakini Ngoswe  anaahidi serikali kuwa sense ijayo kutokuvurunda tena.

·         Mgogoro kati ya mitomingi na serikali, chanzo cha mgogoro huu kilitokea baada ya uamuzi wa mitomingi wa kuchoma moto kazi ya sense. Kwa sababu Ngoswe alimtorosha bintiye suluhisho la mgogoro huu lilikuwa mitomingi kuahidi serikali kuwa hatarudia makosa hayo.

·         Mgogora kati ya mitomingi na wakeze, mgogoro huu uliyotokea baada ya mazoea kutoroshwa na Ngoswe, mitomingi anahisi wakeze walijua jambo hili suluhisho la mgogoro huu ulikuwa mitomingi kuwadharirisha wakeze kuwa akili zao ni saw ana za watoto hali hii iliwa dharirisha wakeze.

·         Mgogoro kati ya mama mazoea na mama linda, mgogoro huu ulitokana na kuingiliana katika malezi ya mazoea kitendo kilichosababisha mazoea kutoroshwa. Hivyo kulijengeka chuki kati ya mama mazoea na mama mainda

  XXXXXMCHAMBUZI MWL MKAMBA. BAED (HONS) UDMS 2009XXXXX
 Inaendelea=======>


Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER MKAMBA EDUCATION CONSULTANCY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment:

Post a Comment