UHAKIKI WA MASHAIRI YA CHEKA CHEKA

 


UHAKIKI WA MASHAIRI YA CHEKA CHEKA

MWANDISHI: THEOBALD A MVUNGI

WACHAPISHAJI: EDUCATIONAL PUBLISHERS AND DISTRIBUTORS LTD

 MWAKA 1995

MCHAMBUZI: MKAMBA

        Msanii wa mashairi ya chekacheka amejadili kwa kina matatizo yanayoikumba jamii yake hasa  yale ya kisiasa. Kama vile rushwa, uhujumu, uchumi, uongozi mbaya, democrasia ya chama kimoja na vyama vingi. Pia amejadili masuala ya mapenzi, dini, ukasuku wa waandishi na mengineyo.

MAUDHUI

DHAMIRA KUU – UMUHIMU WA KUWEPO KWA UONGOZI BORA KATIKA JAMII

       Mwandishi ameonyesha sifa za uongozi bora kuwa ni wale wanaosema ukweli bila uongo na bila kuwapa wahujumu uchumi mafuta kwa mgongo wa chupa katika shairi la “kazi yetu harakati” amebainisha kuwa viongozi bora lazima  wawe wakweli. Pia democrasia ya kweli ni ile inayojali haki za wananchi na kuwapa watu uhuru wa kuamua mambo yao wenyewe katika shairi la taifa “wamelizika”anaetaka jamii iwe na demokrasia ya vyama vingi badala ya chama kimoja cha siasa.

                   “Waogopa vingi vyama, ni hofu ya kuumbika

                     Maovu wanayafuma, kwa dharau na dhikika

                     Vyama vingi vinasema , na kutwaa madaraka

Pasipo uhuru huo, utu upo mashakani.

Hivyo msanii anatuonesha jinsi mfumo wa chama kimoja unavyficha maovu ya viongozi katika jamii yetu. Hivyo basi msanii anataka uongozi bora wenye  kukemea maovu kama vile usaliti, matabaka na unyonyaji ili kuleta maendeleo ya kweli katika

 

DHAMIRA NDOGONDOGO

1.      USALITI

Msanii anaona kuwa kuna baadhi ya viongozi ambao ni wasaliti hasa pale wanapofunga mali ya umma wakiwaacha wananchi wakiteseka na hali duni ya maisha katika shairi la      “kuna nini huko ndani” msanii anasema.

                                      ‘Tumewaletea kuni, maharage hata unga,

                                        Halafu mnatuhiki, marafikizo mwahonga,

                                        Mwataka tulale chini,mturese mkiringa,

Hizo kofia nyeupe, tumewaazima sisi.

Hapa mshairi anawauliza wapishi kuwa wanapika halafu wanakula wenyewe.

 

2.      SUALA LA MATABAKA

Msanii ameona kuwa katika jamii yake kuna matabaka yaani tabaka tawala (viongozi) na tabaka tawaliwa (wananchi) msanii anadhihirisha hili katika mashairi ya “utu umekuwa kima” mashairi ya ngulu. Tabaka tawala linanyanyasa na kunyonya tabaka la chini.

 

3.      UONGOZI MBAYA

Uongozi mbaya ni kiwazo cha kuleta mageuzi na maendeleo katika jamii.

Msanii anaona kuwa uongoziulioko madarakani haujali wananchi na wanajilimbikiza mali.Mashairi yafuatayo yanashadadia dhamira hii. “Chura amegundulika” “utaliwa kama punda”, “Chunguzeni walio mbele”, muwapinawauliza?”

4.      UKWELI NA UWAZI KATIKA JAMII

Mwandishi anataka viongozi wakweli wasio na woga katika kuwafichua wahujumu uchumi katika shairi la “mwinyi ume………………………katika shairi la “kweli ilojaa udi”

                                “Ati ni maendeleo, mana watu wamezidi,

                                 Hakuna kasema siyo, kweli uliyojaa udi,

                                 Kweli yenye kivutio, kweli yenye ustadi,

Hukuna dongo namito, wala watu na mipango.

Hivyo msanii anataka viongozi kuwa wakweli hasa pale matatizo yanapotokea wasidanganye  wanamili na wametayali kufichua maovu katika jamii.

 

5.      DEMOKRASIA

Msanii anaamini kuwa demokrasia ya mfumo wa chama kimoja ni chanzo cha viongozi kuficha maovu katika shairi la “Taifa wamelizika “ msanii anasema .

                                “Mmezikwa demokrasi, chama kimoja ndoo ngao,

                                 Watu hawana nafasi , kutetea nchi nyao,

                                  Mawazo ya ukakasi, mawazo ya mtitio

                                 Wapenda jibu mkato, wale woga wa hoja.

 

                                 “Waogopa vingi vyama, ni hofu ya kuumbuka,

                                  Maovu wanayotuma, kwa dharau na dhikika,

                                  Vyama vingi vinasema, na kutwaa madaraka,

Pasipo uhuru huo, utu upo mashakani.

Hapa msanii anaonyesha jinsi viongozi wanavyoogopa mfumo wa vyama vingi. Kwa hofu ya kuumbuka. Hivyo naamini kwamba siasa ya mfumo wa vyama vingi ndio suruhisho pekee la matatizo nchini Tanzania.

XXXXXMCHAMBUZI MWL MKAMBA. BAED (HONS) UDMS 2009XXXXX

 Inaendelea=======>

 

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER MKAMBA EDUCATION CONSULTANCY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment:

Post a Comment